Thursday 28 February 2013

Dorothy Nyambu a.k.a Dotty akanusha kile ambacho wenzake wanakieneza kuwa mchumba wake anamzuia kuendeleza talanta yake.Anasema amekuwa na mwito mkubwa kwenye safu hii ya filamu na kila mmoja anataka aende mbele hata mchumba wake pia.Dotty ambaye aliwahi onekana kwa mara ya kwanza katika filamu ya MUME NI KAZI iliyotayarishwa na Ogutu Atata chini ya Heartland kenya,anashukuru familia yake kumpa support kubwa na tayari anatayarisha filamu nyingine kwa jina UZITO WA HISIA ambayo ananuia kufanya vizuri zaidi."nimejifunza mengi hasa wakati tukiwa kwenye mazoezi na sasa naja na mbwembwe za hali ya juu"asema Dotty

No comments:

Post a Comment